Posts

Showing posts from December, 2023

Vyakula Vitakavyosaidia Kuilinda Afya ya Figo yako..!!!

Image
Afya ya figo ni muhimu kama ilivyo afya ya moyo, hii ni kwa sababu figo ni moja ya kiungo ambacho husaidia kuchuja sumu mbalimbali ndani ya mwili na baadaye kutoa taka mwili kwa njia ya haja ndogo (mkojo) Matatizo ya figo huweza kuchangia ugumu wa upatikanaji wa haja ndogo (mkojo) au miguu na mikono kuvimba. Pia mtu mwenye shida ya figo huwa katika hatari kubwa ya kukumbwa na matatizo ya moyo. Ulaji unaofaa mara zote husaidia sana kulinda afya ya viungo vyote muhimu ndani ya mwili ikiwa ni pamoja na figo na kuifanya iweze kufanya kazi zake vizuri ndani ya mwili. Hata hivyo, kuna baadhi ya vyakula ambavyo tunaweza kusema ni vyakula rafiki kwa afya ya figo ndani ya mwili ni vyema ukafahamu hapa leo. Karibu>>> Kabeji, hii ni mboga ambayo wengi wetu tunaifahamu sana na tumekuwa tukiitumia katika maisha yetu ya kila siku, lakini ni vyema msomaji wangu ukatambua kwamba mboga hii nayo inauwezo mzuri wa kulinda afya ya figo yako. Samaki pia ni muhimu sana kwa afya ya figo, hii ni kwa ...

Mambo ya Kufanya Pale Simu au Tableti Yako Ikilowa au Kuingia Kwenye Maji

Image
Ulikuwa umeishika vibaya na ikakuponyoka na kuangukia kwenye beseni..au kwenye dimbwi la maji… au kwenye sehemu ya kuogelewa (Pool).. Hizo ni baadhi tuu ya maeneo ambayo yanaweza sababisha simu au tableti yako kukutana na maji. Jambo ambalo linaweza sababisha kufa kwa kifaa chako cha bei nono! Mara nyingi jambo la kwanza atakalofanya mtu ni kuhangaika kufuta maji hayo mara moja…. iwe kwa kutumia nguo yake, au chochote kile cha karibu. Ila je ni sahihi? HAPANA! Hatua ya 1: Itoe mara moja kwenye maji. Inavyozidi kukaa kwenye maji muda mrefo ndivyo uwezekano wa kupona katika janga hili unakuwa mdogo zaidi. Imedondoka kwenye choo? Hapo itakubidi ufanye maamuzi ya haraka kama utaichomoa haraka au uisahau kabisa. Utafanya nini? Hatua ya 2: Bila kupoteza muda izime mara moja! Na kama ni simu yenye eneo la kutoa betri basi usitumie switchi yake kuzimia, bali toa betri mara moja.  Usajaribu kubonyeza kingine chochote , ondoa betri . Na kama ni tableti au simu za iPhone ambazo hazina sehemu ...

Mambo 8 Muhimu ya Kuzingatia kutoka Kuajiriwa Hadi Kujiajiri

Image
Kuna sababu mbalimbali kwanini mtu atake kuajiri, badala ya kuajiriwa, mfano kipato kidogo anachopata katika kazi husika, hitaji la kutaka uhuru zaidi binafsi wa kufanya kazi, hitaji la kuweza kutoa ajira kwa wengine na zaidi sana kuweza kutumia vema kipaji na uwezo wa kuzalisha ambao katika kazi ya sasa mtu hapati nafasi ya kufanya hivyo. Kujiajiri ni jambo linalohitaji maandalizi ya muda mrefu na kuna mambo ya msingi kuyafahamu, haiwezekani tuu , ukaacha kazi na kusema ok, acha nijiajiri. Makala hii inachambua mambo ya msingi ya kujiandaa na kuyafahamu kabla mtu hajaamua kuacha kuajiriwa. Mkakati ni muhimu Wazo au ndoto isiyo na mkakati wa kuitimiza ni upuuzi yaani ndoto hiyo au wazo hilo halina maana, hivyo basi ndoto yako ya kujiajiri siku moja, ni lazima iwekewe mkakati wa kuifanikisha ikiwa ni pamoja na muda hasa wa lini utaitimiza hiyo ndoto. Katika kuweka mkakati huu wa kutimiza ndoto yako, fanya utafiti wa kina kuhusu mipango yako binafsi ya maisha, mtazamo wako kuhusu maisha,...

Jifunze namna ya kulainisha viganja au mikono

Image
Moja ya hasara ya mwanamke aliye hodari na kazi za nyumbani ni viganja vya mikono kuwa vigumu au vikavu. 🎀Kama unafua na maji na sabuni, kuosha vyombo, kusafisha nyumba, kubadili watoto nepi au diapers,kupika n.k . usishangae kuwa na viganja vigumu au vikavu. 🎀Hakuna haja ya kuogopa na toa wasiwasi hii ni aina ya kufanya mikono yako iwe laini na ya kuvutia.  _ 🎀Huna haja ya kwenda kwa spa’s wala kwa wataalamu. Baada ya kazi zako fanya haya; 🕸Kunywa maji kwa wingi na kisha tumia njia hizi zifuatazo; 🕸Chukua container weka chumvi kiasi. 🕸Weka olive oil ndani ya container.  _ 🕸Weka sabuni ya maji ya kuoshea mikono, tumia aina unayoipenda inaweza kuwa anti-bacterial au yoyote ya maji. Ni vizuri kutumia sabuni ya maji,  sababu ya kawaida hautaosheka vizuri mkono sababu maji na mafuta hayachanganyiki.  _ 🕸Kausha mikono yako vizuri, kisha weka mchanganyiko huo kwenye viganja vyako kiasi cha ½ kijiko cha chai kisha sugua pole pole. Sugua ndani na nje ya viganja na nd...

Mbinu za asili za kuongeza nguvu za kiume

Image
Upungufu wa nguvu za kiume umekua tatizo kubwa sana kwa wanaume wengi. Tatizo hili limewakumba wanaume wengi walio katika ndoa na hata wale ambao bado hawajaoa. Watu wengi wamekuwa wakisumbuka kutafuta utatuzi kwani tatizo hili huwafanya kuwa na wasiwasi wa maisha. Ndoa nyingi zimevunjika na mahusiano kuharibika kwa sababu ya tatizo hili. Kwa wanaume wenye umri mkubwa, upungufu wa nguvu za kiume unaweza usiwe ni tatizo kwani miili yao inakuwa tayari imechoka. Hizi hapa ni baadhi ya njia zitakazokusaidia kurudisha nguvu za kiume zilizokuwa zimepotea, au kuimarisha uwezo wako wa tendo la ndoa. Jitahidi kutumia vinywaji na vyakula visivyokuwa na sukari nyingi. Epuka vinywaji vyote vyenye sukari nyingi kwani ni adui mkubwa sana wa afya yako hasa wakati unataka kurudisha nguvu za kiume. Kula vyakula asili na nafaka ambayo haijakobolewa, kula matunda kwa wingi pamoja na mboga za majani. Utafurahia maisha ya kula vyakula asili na utakuwa imara katika tendo la ndoa. Epuka unywaji wa Pombe. Taf...

Faida saba(7) zitokanazo na juisi ya ukwaju

Image
Juisi ya ukwaju ina umuhumi sana katika miili yetu, pia tunda la ukwaju ni tunda lenye faida nyingi sana kwa afya ya mwanadamu. Tunda hili huweza kutumika kutengeneza juisi ambayo matumizi yake yana faida kubwa sana katika afya ya mwili wa mwanadamu. Zifuatazo ndizo faida zitokanazo na juisi ya ukwaju; 1. Chanzo kizuri cha viuasumu mwilini ‘antioxidants’ ambavyo huzuia Saratani (cancer) kwa mtumiaji 2. Chanzo cha Vitamini B na C vile vile “carotentes” 3. Hushusha joto la mwili na kuondosha homa, hasa homa ya malaria na homa ya matumbo 4. Huulinda mwili dhidi ya mafua na kero za mafua kooni 5. Husaidia myeyusho na mmengenyo wa chakula na kuondosha kuvimbiwa 6. Husaidia kutibu matatizo ya nyongo (bile disorders) 7. Husaidia kurahisisha choo (laxative) 8.Husaidia kupunguza wingi wa lehemu (cholesterol) na hivyo kuimarisha moyo 9.Husaidia ngozi kuwa nyororo, vile vile husaidia ngozi inayopona baada ya kuungua au yenye vidond 10.Husaidia kuua minyoo tumboni (kwa watoto wadogo) Hizi Ndiyo Fa...

Unafahamu Umuhimu wa Tende Mwilini..? Jibu Liko Hapa..!!!

Image
Tende ni tunda ambalo linayeyuka kirahisi tumboni na lenye faida nyingi sana ambazo hulifanya liwe tunda la kipee.  Zifuatazo ni faida ya tunda la tende katika mwili wa binadamu.  Kwa watu wenye matatizo ya tumbo, nicotinic inayopatikana kwenye tende husaidia kurekebisha matatizo ya tumbo na huleta ahueni kwa watu wenye matatizo ya kupata choo.  Tende husaidia kuuimarisha moyo. Iloweke tende kwenye maji kwa usiku mmoja na asubuhi kunywa maji hayo pamoja na tende zilizolewekwa baada ya kuondoa mbegu, ukifanya hivyo mara mbili kwa wiki, moyo wako utakuwa imara.  Tende husaidia pia kwenye mambo ya malavi davi. Iloweke tende kwenye maziwa ya mbuzi usiku, asubuhi changanya maziwa hayo na asali kisha kunywa, njia hii husaidia kuongeza nguvu na stamina.  Utafiti umeonyesha kuwa tende husaidia kutanua misuli ya mji wa mimba wakati mwanamke anapokaribia kujifungua, hii husaidia kumfanya mwanamke asipoteze damu nyingi wakati wa kujifungua.  Wataalamu wa vyakula, wana...